Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 32:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Ikiwa watu wa Gadi na wa Rubeni watavuka muto Yordani pamoja nanyi wakiwa na silaha zao chini ya uongozi wa Yawe, mukishinda na kuitwaa inchi hiyo, basi mutawapa inchi ya Gileadi ikuwe mali yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 32:29
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini sisi wenyewe tutatwaa silaha zetu tayari kwenda kwa vita pamoja na wandugu zetu Waisraeli, na tutakuwa kwa mustari wa mbele katika vita mpaka tuwafikishe pahali watakapokaa. Wakati huo watoto wetu watakaa kwenye miji yenye kuta, kwa kujilinda na wenyeji wa inchi hii.


Basi, Musa akatoa amri hizi kwa kuhani Eleazari, kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa jamaa za makabila ya Waisraeli:


Lakini kama hawatavuka muto Yordani pamoja nanyi na silaha zao, basi watarizi sehemu ya inchi ya Kanana pamoja nanyi.


Musa mutumishi wa Yawe pamoja na Waisraeli aliwashinda wafalme hao, akawapatia inchi hizo makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase zikuwe mali yao kabisa.


pamoja na inchi za Gileadi, eneo la Wagesuri na Wamakati mulima wa Hermoni na inchi yote ya Basani mpaka Saleka;


Musa alikuwa ameyapa yale makabila mawili na nusu sehemu yao upande wa mashariki wa Yordani, lakini Walawi hawakukuwa wamepewa sehemu yao pamoja nao.


Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”


Basi, watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakaachana na watu wa makabila mengine ya Israeli kule Shilo katika inchi ya Kanana, wakarudi kwao katika inchi ya Gileadi, inchi yao wenyewe walioirizi kwa amri ya Yawe kama vile alivyomwagiza Musa.


Nyuma ya Tola, kukatokea Yairi wa Gileadi, akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka makumi mbili na mbili.


Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ