Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 32:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 32:23
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”


Yuda akamujibu: “Tukuambie nini bwana? Tuseme nini kwa kuonyesha kwamba hatuna kosa? Mungu ameyafichua makosa yetu, sisi watumishi wako. Sasa sisi wote tuko watumwa wako, sisi pamoja na yule aliyepatikana na kikombe chako.”


Ijapokuwa mumenipakaa mafuta kusudi nikuwe mufalme, lakini leo mimi ni zaifu. Hawa wana wa Zeruya ni wakali kupita kipimo. Yawe awaazibu waovu hawa sawasawa na uovu wao.”


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Azabu ya mauaji hayo itakuwa juu ya Yoabu na wazao wake milele. Lakini Yawe atawabariki siku zote Daudi na wazao wake watakaoikalia kiti chake cha kifalme.”


Kama ningeliomba giza linifunike, giza linizunguke pahali pa mwangaza,


Makaa ya moto yawaangukie; watumbukizwe katika mashimo, wasiinuke tena.


Maovu yetu umeyaweka mbele yako; zambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.


Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.


maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena, lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Makosa yetu mbele yako ni mengi sana, zambi zetu zinashuhudia juu yetu. Kweli, makosa yetu yanaandamana nasi, tunayajua maovu yetu.


Kisha wale watumishi wa mashua wakasemezana: Tupige kura tupate kujua hasara hii imetupata kwa ajili ya kosa la nani. Basi, wakapiga kura; kura ikamwangukia Yona.


Mateso na taabu zitamupata kila mutu anayefanya mabaya: kwanza Wayuda, kisha watu wa mataifa mengine vilevile.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Yoshua akaileta jamaa ya Zabedi karibu, nyumba kwa nyumba; na nyumba ya Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, ikachaguliwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ