Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 31:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uwalipize kisasi Wamidiani mambo waliyowatendea Waisraeli; kisha wewe utakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 31:2
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wewe mwenyewe utaishi maisha marefu na kufa kwa amani.


Isimaeli alikuwa na umri wa miaka mia moja makumi tatu na saba alipokufa na kukutana na wazee wake.


Kisha kuishi maisha marefu na ya fanaka, akakufa na kukutana na wazee wake.


Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.


Haruni atakufa; hataingia katika inchi ambayo nimewapa Waisraeli kwa sababu ninyi wawili muliasi amri yangu kule Meriba.


Kisha, umuvue Haruni nguo yake, umuvalishe mwana wake Eleazari. Haruni atakufa akiwa huko kwenye mulima.


Waisraeli walipokuwa kule Sitimu, wanaume wakaanza kuzini na wanawake wa Moabu.


Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.


Ukisha kuiona, utakufa na kukutana na wazee wako, kama vile ndugu yako Haruni alivyokutana nao,


Basi Musa akazungumuza na watu akawaambia: Mutayarishe watu kwa vita waende kuwashambulia Wamidiani kwa kumulipizia Yawe kisasi.


Kwa maana siku zile zitakuwa siku za azabu ya Mungu, kusudi mambo yote yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yatimie.


Lakini Daudi alipokwisha kutumika sawasawa na kusudi la Mungu katika maisha yake, akakufa na kwenda kukutana na babu zake waliomutangulia, naye akaoza.


Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”


maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.


Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.


Mimi nitakufia katika inchi hii wala sitauvuka muto, lakini ninyi muko karibu kuuvuka na kwenda kurizi inchi ile nzuri.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Kwa maana tunamujua yule aliyesema: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.” Naye alisema tena: “Bwana atawahukumu watu wake.”


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


Watu walipomwona Samusoni wakamusifu mungu wao na kusema: “Mungu wetu amemutia adui yetu katika mikono yetu ambaye alikuwa akiharibu inchi yetu na kuwaua wengi kati yetu.”


Kisha watu wote wa kizazi chake wakakufa, kizazi kingine kikafuata ambacho hakikumujua Yawe wala matendo aliyowatendea watu wa Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ