Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Watatunza vyombo vyote vya hema la mukutano na kuwasaidia Waisraeli wanapofanya kazi zao kwenye hema takatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 3:8
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kulingana na maagizo ya mwisho Daudi aliyotoa, Walawi wote waliofikia umri wa miaka makumi mbili waliandikishwa.


Basi wana wangu, musikuwe wavivu. Yawe amewachagua ninyi kusudi mumutumikie, muwaongoze watu wake katika ibada, na kumufukizia ubani.”


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Kisha, hema likashushwa, na watu wa ukoo wa Gersoni na wa Merari ambao walilibeba, walianza kuondoka.


Kisha walifuata watu wa ukoo wa Kohati, wakiwa wamebeba vyombo vitakatifu. Walipofika, hema lilikuwa limekwisha kusimikwa.


Watafanya kazi kwa pahali pake na pa Waisraeli wote pamoja kwenye hema la mukutano wanapotumika pale.


Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.


Kutoka katika lile fungu la jamii nzima, utwae mumoja kati ya kila makumi tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo na mbuzi. Hivyo utawapa Walawi ambao wanashugulika na kazi katika hema la Yawe.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Hii ndiyo kazi ya jamaa za Gersoni kwenye hema la mukutano; watafanya kazi chini ya uongozi wa Itamari mwana wa kuhani Haruni.


Hii ndiyo itakayokuwa kazi ya wana wa ukoo wa Merari katika utumishi wao wote ndani ya hema la mukutano, chini ya uongozi wa Itamari mwana wa kuhani Haruni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ