Kisha Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme akamupeleka Seraya, Kuhani Mukubwa, kuwa mufungwa pamoja na Zefania, kuhani wa pili, na wakubwa wa walinda milango watatu.
Wao walioshugulika na kazi ya kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, mazabahu, vyombo makuhani wanavyotumia hema takatifu na pazia; kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.
Eleazari mwana wa kuhani Haruni atatunza mafuta ya taa, ubani wa kufukiza, sadaka za vyakula za kila siku, mafuta ya kupakaa kwa kutakasa na kila kitu kilichotakaswa katika hema hilo.
Haruni na wana wake makuhani ndio watakaoamrisha kazi zote za Wagersoni juu ya vitu watakavyobeba na kazi watakazofanya. Utawapangia vitu vyote vile ambavyo wanapaswa kubeba.
Lakini, anaweza kuwasaidia Walawi wenzake wanapotumika katika hema, lakini haruhusiwi kufanya kazi yoyote peke yake. Ndivyo utakavyowapangia Walawi kazi.