Kisha uwapakae mafuta kama vile ulivyomupakaa baba yao, kusudi nao vilevile wanitumikie kama makuhani. Kupakwa mafuta huku kutawaingiza katika ukuhani wa kudumu katika vizazi vyao vyote.
Halafu Musa akatwaa mafuta ya kupakaa na damu kutoka mazabahu akamunyunyizia Haruni na wana wake hata na nguo zao vilevile. Hivyo Musa akamutakasa Haruni na wana wake pamoja na nguo zao.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya Yawe, wakati walipomutolea Yawe moto usiokuwa mutakatifu katika jangwa la Sinai. Wao hawakukuwa na watoto. Kwa hiyo Eleazari na Itamari wakatumika kama vile makuhani chini ya uongozi wa baba yao Haruni.
Sheria ya Musa inawaweka watu wenye uzaifu kuwa Makuhani Wakubwa, lakini kufuatana na kiapo kilichokuja nyuma ya Sheria ile, Mwana anayekuwa mukamilifu kwa milele aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa.