Hesabu ya Walawi kulingana na jamaa zao, wanaume wote kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ambao Musa na Haruni waliwahesabu kwa amri ya Yawe, ilikuwa watu elfu makumi mbili na mbili.
Haruni na wana wake makuhani ndio watakaoamrisha kazi zote za Wagersoni juu ya vitu watakavyobeba na kazi watakazofanya. Utawapangia vitu vyote vile ambavyo wanapaswa kubeba.
Hii ndiyo hesabu ya watu wa jamaa ya Wakohati, ambao walitumika katika hema la mukutano, ambao Musa na Haruni wakawahesabu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Hii ndiyo iliyokuwa hesabu ya watu wa jamaa za wana wa Gersoni wote waliotumika katika hema la mukutano, ambao Musa na Haruni waliwahesabu kama vile Yawe alivyowaamuru.
Nao makuhani wa ukoo wa Lawi sharti wakuwe pale. Yawe, Mungu wenu, aliwachagua wamutumikie na kubariki kwa jina lake. Wao vilevile ndio wenye mamlaka ya kuamua magomvi na maneno juu ya kuumizana.