Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.
Hesabu ya Walawi wanaume wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na tatu. Hawa hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu wao hawakupewa urizi wowote kati yao.
hizi ndizo jamaa za Merari. Hesabu yao kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa watu elfu sita na mia mbili.
Wote wazaliwa wa kwanza wanaume kadiri ya hesabu ya majina, kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi, kufuata jinsi walivyohesabiwa, walikuwa elfu makumi mbili na mbili mia mbili makumi saba na tatu.
Yesu alipoona vile, akakasirika na kuwaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.