Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.
Kutakuwa siku sita za kufanya kazi. Lakini siku ya saba ni Sabato. Siku hiyo ni ya mapumziko, hamutafanya kazi na mutakuwa na mukutano mutakatifu. Siku hiyo ya saba hamutafanya kazi. Hiyo ni Sabato ambayo ni takatifu kwangu mimi Yawe katika makao yenu yote.
Kwa muda wa siku hizo zote saba mutanitolea mimi Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto. Katika siku ya saba mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi.
Katika siku sita mutakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya saba kutakuwa mukutano mukubwa wa kumwabudu Yawe, na hamutafanya kazi yoyote katika siku hiyo.