Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 28:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akamwambia Musa:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 28:1
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.


Nyumba ninayokusudia kujenga itakuwa kubwa sana, maana Mungu wetu ni mukubwa zaidi ya miungu yote.


Kuhani Yoyada akaweka walinzi kwa kulinda nyumba ya Yawe. Hao walinzi wakasimamiwa na makuhani na Walawi ambao Daudi aliwaweka katika kazi ya kutunza nyumba ya Yawe kutoa sadaka za kutetezwa kwa moto kwa Yawe kama vile ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, wakishangilia na kuimba kwa kufuata amri ya Daudi. Vilevile wakasimamia mambo ya uimbaji na sherehe.


Kutoka mali yake mwenyewe, mufalme akatoa sehemu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa asubui na magaribi, za siku ya Sabato na wakati wa sherehe za mwandamo wa mwezi na zile sikukuu zingine zilizoamuriwa kulingana na Sheria ya Yawe.


Alitoa sadaka zile kadiri ilivyotakiwa na amri ya Musa kila siku takatifu, ni kusema siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, na sikukuu tatu za kila mwaka – sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, sikukuu ya majuma na sikukuu ya vibanda.


Kila siku, tena bila kukosa, mutawapa makuhani wa Yerusalema kila kitu watakachohitaji; ikuwe ni ngombe dume, wana-ngombe, kondoo dume au wana-kondoo wa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Mungu wa mbinguni, au ngano, chumvi, divai au mafuta.


Tunajiwekea sheria juu yetu kwamba, kwa mwaka tutatoa sehemu moja ya tatu ya kikoroti kimoja cha feza kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu:


Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.


Kukikuwa magombano wataamua kadiri ya maamuzi yangu. Katika sikukuu zote watafuata sheria zangu na maamuzi yangu, na kuzitakasa Sabato zangu.


Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.


Wakati wa siku za sikukuu na siku zilizopangwa, sadaka za unga zitakuwa litre kumi na saba zikiandamana na kila ngombe dume au kondoo dume, na chochote ambacho anayeabudu anaweza kutoa kwa kila mwana-kondoo. Kwa kila sadaka ya unga atatoa litre tatu za mafuta.


Kisha, Haruni akaleta mbele sadaka ya watu. Akatwaa mbuzi wa sadaka ya watu kwa ajili ya zambi, akamuchinja na kumutoa sadaka kwa ajili ya zambi, kama vile alivyofanya kwa yule wa kwanza.


Kisha akamwekea mikono juu ya kichwa na kumupa mamlaka kama vile alivyoagizwa na Yawe.


Uwaamuru Waisraeli maneno haya: Ninyi mutanitolea kwa wakati wake sadaka zinazotakiwa: vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza.


Kwa nini munashugulika na kutimiza desturi zenu za siku, miezi, nyakati na za miaka?


Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ