Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.
Halafu Solomono akaikaa katika kiti cha kifalme cha Yawe, kwa pahali pa baba yake Daudi. Naye akafanikiwa; na taifa lote la Waisraeli likamutii. 29.23 Ang. 1 Fal 2.12
Yawe akamupa Solomono sifa nzuri mbele ya Waisraeli wote, akamupa utukufu wa kifalme unaopita utukufu wa mufalme yeyote aliyeitawala inchi ya Israeli mbele yake.
Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.
Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.