Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 27:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 27:17
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”


Halafu, Mikaya akasema: “Niliona watu wote wa Israeli wametawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi. Basi warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Ee Yawe, Mungu wangu, umeniweka mimi mutumishi wako kuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, ijapokuwa ningali mutoto mudogo na sijui namna ya kutimiza kazi hii.


Mutamuzunguka mufalme, kila mutu na silaha yake katika mukono na mutu yeyote atakayesubutu kuwakaribia mumwue. Mukae na mufalme, ikiwa anatoka au anaikaa.”


Kwa hiyo, ninakuomba unipe hekima na maarifa kusudi niweze kuwatawala watu wako vizuri. Kama sivyo, nitaweza namna gani kuwatawala hawa watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


Naye Mikaya akasema: “Niliwaona watu wote wa Israeli wakitawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi; uwaache warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Basi, kwa sababu hao kondoo hawakuwa na muchungaji, walisambazwa na kuwa chakula cha nyama wa pori.


Sanamu zao za kupigia ramuli ni uongo mutupu, na waaguzi wao wanaagua uongo; watabiri wao wanatabiri ndoto danganyifu, na kuwapa watu faraja za bure. Ndiyo maana watu wa Yuda wanatangatanga kama kondoo; wanataabika maana wamekosa muchungaji.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Lakini muwaendee wandugu zenu wa inchi ya Israeli, wanaokuwa kama kondoo wanaopotea.


Naye Yesu akajibu: “Nimetumwa tu kwa taifa la Waisraeli, wanaokuwa kama kondoo wanaopotea.”


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


akawaambia: “Mimi sasa nina umri wa miaka mia moja na makumi mbili, na sina nguvu ya kufanya kazi zaidi. Tena Yawe ameniambia kwamba sitavuka muto Yordani.


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Hivyo, Saulo akamwondoa na kumufanya kiongozi wa waaskari elfu moja. Naye Daudi akawaongoza vyema katika vita.


kusudi nasi vilevile tukuwe sawa mataifa mengine. Mufalme wetu, atatuamulia haki zetu, atatuongoza na kutupigania vita vyetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ