Mutamuzunguka mufalme, kila mutu na silaha yake katika mukono na mutu yeyote atakayesubutu kuwakaribia mumwue. Mukae na mufalme, ikiwa anatoka au anaikaa.”
Halafu, mufalme Zedekia alimwapia Yeremia kwa siri akisema: Kama vile Yawe, yule aliyetupatia uzima, anavyoishi, sitakuua wala sitakutia katika mikono ya hawa wanaotaka kukuua.
Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?
Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.
Yawe akamwambia Musa: “Siku yako ya kuaga dunia imekaribia. Umwite Yoshua, mukuje pamoja katika hema la mukutano kusudi nimupe maagizo.” Basi, Musa na Yoshua wakaenda katika hema la mukutano,
Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?