Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 27:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 kwa sababu hamukuitii amri yangu kule katika jangwa la Sini, wakati watu wote pamoja waliponigombanisha kule Meriba. Ninyi hamukuacha utukufu wangu uonekane mbele yao walipotaka wapewe maji. (Meriba ni chemichemi ya maji ya Kadesi katika jangwa la Sini).

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 27:14
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”


Basi, watu hao wakaenda na kupeleleza inchi toka jangwa la Sini mpaka Rehobu, karibu na njia ya kuingilia Hamati.


Waisraeli wote wakafika katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza, wakapiga kambi yao huko Kadesi. Wakiwa huko, Miriamu akakufa na kuzikwa.


Haruni atakufa; hataingia katika inchi ambayo nimewapa Waisraeli kwa sababu ninyi wawili muliasi amri yangu kule Meriba.


Kwa nini mulitutoa Misri na kutuleta pahali hapa pabaya hivi? Hapa si pahali pa ngano, tini, zabibu wala makomamanga. Hata maji ya kunywa hakuna!


“Ninyi watu wagumu! Ninyi wenye roho ya kipagani na masikio yanayofungana! Siku zote munapingana na Roho Mutakatifu sawa vile babu zenu walivyofanya!


Yawe akanikasirikia mimi vilevile kwa sababu yenu, akasema: ‘Hata wewe Musa hautaingia katika inchi hiyo.


Mimi nitakufia katika inchi hii wala sitauvuka muto, lakini ninyi muko karibu kuuvuka na kwenda kurizi inchi ile nzuri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ