Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 26:62 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

62 Hesabu ya Walawi wanaume wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na tatu. Hawa hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu wao hawakupewa urizi wowote kati yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 26:62
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Walawi hawakuhesabiwa pamoja na yale makabila mengine,


Usifanye hesabu ya kabila la Lawi pamoja na ile ya watu wa Israeli.


Hao ndio wanaume Waisraeli waliohesabiwa na Musa na kuhani Eleazari katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya muto Yordani, karibu na Yeriko.


Hesabu ya Walawi kulingana na jamaa zao, wanaume wote kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ambao Musa na Haruni waliwahesabu kwa amri ya Yawe, ilikuwa watu elfu makumi mbili na mbili.


Haruni na wana wake makuhani ndio watakaoamrisha kazi zote za Wagersoni juu ya vitu watakavyobeba na kazi watakazofanya. Utawapangia vitu vyote vile ambavyo wanapaswa kubeba.


kwa jumla walikuwa watu elfu nane na mia tano na makumi nane.


Ndiyo maana kabila la watu wa Lawi halina sehemu ya inchi ya urizi pamoja na wandugu zao. Walichopokea ni heshima ya kuwa makuhani wa Yawe, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyoahidi.)


Musa hakuwapa watu wa kabila la Lawi inchi yoyote. Lakini sadaka za kuteketezwa kwa moto walizomutolea Yawe, Mungu wa Israeli, hizo ndizo zilizokuwa fungu lao, kama vile Yawe alivyomwambia Musa.


Lakini kabila la Lawi, Musa hakulipa sehemu yao ya inchi, maana aliwaambia kwamba sehemu yao itakuwa kumutumikia Yawe, Mungu wa Israeli.


Musa alikuwa ameyapa yale makabila mawili na nusu sehemu yao upande wa mashariki wa Yordani, lakini Walawi hawakukuwa wamepewa sehemu yao pamoja nao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ