61 Nadabu na Abihu walikufa walipomutolea Yawe sadaka ya moto usiofaa.
Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya Yawe, wakati walipomutolea Yawe moto usiokuwa mutakatifu katika jangwa la Sinai. Wao hawakukuwa na watoto. Kwa hiyo Eleazari na Itamari wakatumika kama vile makuhani chini ya uongozi wa baba yao Haruni.