Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 26:53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

53 Makabila haya yatagawanyiwa inchi ikuwe urizi wao, kulingana na hesabu ya majina yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 26:53
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Alisema: “Nitawapa inchi ya Kanana, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”


Aliwapa inchi za mataifa na kuwatolea mashamba ya wenyeji,


Hayo ndiyo yanayowapata wanaojitumainia kwa upumbafu, ndio mwisho wa wale wanaojivunia mali zao.


Mutaigawanya kuwa mali yenu. Wageni watakaokaa kati yenu, wale watakaozalia watoto kati yenu, wapewe vilevile sehemu ya inchi munapoigawanya. Hao wanapaswa kutendewa kama wanainchi wa Israeli na wana haki ya kupiga kura kwa kupata sehemu ya inchi pamoja na makabila ya Waisraeli.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Kabila kubwa litapewa sehemu yao kubwa na dogo litapewa sehemu yao ndogo. Kila kabila litapewa urizi wake kulingana na hesabu ya watu wake.


Mutagawanya inchi hiyo kwa kura kufuata jamaa zenu; eneo kubwa kwa kabila kubwa na eneo dogo kwa kabila dogo.


Heri wale wanaokuwa wapole, maana watarizi dunia!


Ukuwe imara na hodari kwa sababu wewe utawaongoza watu hawa kuirizi inchi ambayo niliwaahidi kwamba nitawapa wazee wao.


Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.


Haya ndiyo maeneo ya inchi ambayo Waisraeli walipewa katika inchi ya Kanana. Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na wakubwa wa ukoo za makabila ya Waisraeli waliyowagawanyia Waisraeli.


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ