52 Kisha Yawe akamwambia Musa:
Hesabu ya wanaume Waisraeli waliohesabiwa ilikuwa elfu mia sita, na moja mia saba na makumi tatu.
Makabila haya yatagawanyiwa inchi ikuwe urizi wao, kulingana na hesabu ya majina yao.
Basi, Musa akawaambia Waisraeli: Hii ndiyo inchi mutakayoirizi kwa kupiga kura, inchi ambayo Yawe ameagiza ipewe kwa makabila tisa na nusu.
Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.
Sehemu hiyo yao waligawanyiwa kwa kura kama vile Yawe alivyomwamuru Musa awape yale makabila tisa na nusu.