Hiramu aliziweka nguzo hizo kwenye baraza ya hekalu; nguzo aliyoisimika upande wa kusini iliitwa Yakini, na ile aliyoisimika upande wa kaskazini iliitwa Boazi.
Haya ndiyo majina ya wakubwa wa jamaa za Waisraeli. Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi. Hao walikuwa babu za jamaa za Rubeni.
Wana wa Simeoni walikuwa: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Sauli. Huyu wa mwisho alikuwa mutoto wa mwanamuke wa Kanana. Hao walikuwa babu za jamaa za Simeoni.