Salumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu, pamoja na wandugu zake wa ukoo wa Kora, walikuwa na kazi ya kutunza viingilio vya hema la mukutano, kama vile babu zake walivyokuwa wakati wa ulinzi wa kambi ya Yawe.
Watu wakaondoka kwenye makao ya Kora, Datani na Abiramu. Datani na Abiramu wakatoka katika mahema yao na kusimama kwenye mulango wakiandamana na wake zao na watoto wao wote hata wale wanaonyonya.
Kisha akamwambia Kora na wafuasi wake: Kesho asubui, Yawe ataonyesha ni nani anayekuwa wake na ni nani anayekuwa mutakatifu, na yule atakayemuchagua, atamuwezesha kukaribia kwenye mazabahu.
na mambo aliyowatendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu, mwana wa Rubeni. Mukumbuke jinsi mbele ya watu wote wa Israeli udongo ulivyofunguka na kuwameza pamoja na jamaa zao, mahema yao, nyama na watumishi wao wote.