Hesabu 26:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Wakati huo udongo ukafunguka ikawameza, wakakufa pamoja na Kora na wafuasi wake moto ulipoangamiza watu mia mbili makumi tano; wakakuwa onyo kwa watu.
Kwa sababu jambo hilo litakalowapata, watu wote waliohamishiwa Babeli kutoka Yuda, watatumia mufano huu kwa kutoa laana: Yawe akufanye kama Zedekia na Ahabu, ambao mufalme wa Babeli aliwachoma katika moto.
Vimekuwa vitakatifu kwa sababu watu hawa walivileta kwenye mazabahu ya Yawe. Basi, utwae vyetezo vya watu hao waliouawa kwa sababu ya zambi zao, vifuliwe kuwa vyembamba kusudi vikuwe kifuniko cha mazabahu. Hili litakuwa onyo kwa Waisraeli wote.
Baba yetu alikufia katika jangwa na bila mutoto yeyote mwanaume. Yeye hakukuwa kati ya wafuasi wa Kora waliokusanyika mbele ya Yawe, lakini alikufa kutokana na zambi yake mwenyewe. Hakukuwa na mutoto mwanaume.
na mambo aliyowatendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu, mwana wa Rubeni. Mukumbuke jinsi mbele ya watu wote wa Israeli udongo ulivyofunguka na kuwameza pamoja na jamaa zao, mahema yao, nyama na watumishi wao wote.
Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.