Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 25:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 25:4
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, utupatie watu saba kati ya wazao wake, nasi tuwatundike mbele ya Yawe juu ya mulima Gibea, kwa Saulo aliyechaguliwa na Yawe.” Mufalme akasema: “Nitawapatia nao.”


Daudi aliwatoa watoto hao saba wanaume kwa Wagibeoni, nao wakawatundika kwenye mulima mbele ya Yawe, wote saba wakakufa pamoja. Watoto hao waliuawa kwa mwanzo wa mavuno ya Shayiri.


Waliichochea hasira ya Yawe kwa matendo yao, magonjwa makali yakatokea kati yao.


Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Finehasi mwana wa Eleazari, mujukuu wa kuhani Haruni, ameizuia hasira yangu juu ya Waisraeli; kati yenu ni yeye tu aliyeona wivu kama ule ninaokuwa nao mimi. Ndiyo maana sikuwaangamiza Waisraeli wote kwa hasira yangu.


kwa sababu waliwachokoza ninyi kwa werevu wao, ambao kwa njia yake wamewadanganya katika jambo la Peori, na kwa sababu ya Kozibi, binti yao, aliyeuawa wakati ugonjwa mukali ulipotokea kule Peori.


Umupige mawe mpaka akufe, kwa sababu amejaribu kukuvuta mbali kutoka kwa Yawe, Mungu wako, ambaye alikutoa toka utumwa katika inchi ya Misri.


“Mutakapoishi katika miji ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa, labda mutasikia


basi mutapeleleza na kufanya uchunguzi na kuuliza kwa uangalifu. Na kama ni kweli kwamba jambo la kuchukiza limetendeka kati yenu,


Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.


“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Ninyi muliona kwa macho yenu mambo ambayo Yawe aliyafanya juu ya Bali-Peori. Yawe, Mungu wenu, aliwaangamiza watu wote kati yenu waliomwabudu huyo mungu Bali-Peori.


Zambi tulizotenda kule Peori hazitoshi? Hamwoni kwamba bado hatujajitakasa na kwamba mateso yake bado yanaisumbua watu wa Yawe?


Yoshua aliwaita Waisraeli wote pamoja na viongozi na wazee wao, waamuzi na wakubwa, akawaambia: “Sasa mimi nimekuwa muzee wa miaka mingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ