Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 24:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Watakuwa na hazina ya kutosha ya maji, mbegu yao itapata maji mengi, mufalme wao atakuwa mukubwa kuliko Agagi, na ufalme wake utatukuka sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 24:7
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivyo, Daudi akatambua kwamba Yawe amemwimarisha akuwe mufalme wa Israeli, na kwamba ameutukuza ufalme wake kwa ajili ya watu wake Waisraeli.


Solomono alitawala falme zote kuanzia kwa muto Furati mpaka katika inchi ya Wafilistini, na kuendelea hata kwa mupaka na Misri. Mataifa yote yalimutumikia na kulipa kodi kwake wakati wote wa maisha yake.


Halafu, Daudi akatambua kwamba Yawe amemwimarisha akuwe mufalme wa Israeli, na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Waisraeli, watu wake.


Wafalme wenye nguvu wamepata kuutawala muji ule pamoja na jimbo la upande wa magaribi wa Furati wakilipisha kodi, malipo ya kuvuka mipaka na mengine.


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Ahasuero akamupandisha Hamani cheo, akakuwa waziri mukubwa. Hamani alikuwa mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.


Niliwatwanga, wakakuwa kama vumbi inayopeperushwa na upepo; niliwakanyaga kama matope katika barabara.


Mbele waimbaji, nyuma wanamuziki, katikati wabinti wanavumisha ngoma.


Wafalme wote wa dunia wamuheshimu, watu wa mataifa yote wamutumikie.


Yeye atasema, ‘Wewe ni baba yangu, Mungu wangu, mulima wa wokovu wangu.’


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Wakati utakapofika ambapo waadui watauawa na minara yao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mulima na kilima.


Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Inchi hiyo imejaa mito na akiba tele, lakini mwisho wake umefika, uzi wa uzima wake umekatwa.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Kisha Balamu akawaangalia Waamaleki, akatoa mashairi haya: Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote, lakini kwa mwisho litaangamia kabisa.


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.


Yule malaika akaniambia tena: “Yale maji uliyoona pale yule kahaba anapoikaa, ni watu wa kila taifa, kila jamaa na kila luga.


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ