Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa Balamu akatambua kwamba Yawe alipenda kuwabariki Waisraeli, kwa hiyo hakukwenda sawa vile mara ingine kwa kutafuta uchawi. Akaelekea kwenye jangwa,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 24:1
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, asubui yake Balamu akaamuka, akawaambia wazee wa Balaki: Murudie katika inchi yenu, kwa maana Yawe hapendi kuniruhusu kwenda pamoja nanyi.


Basi, wazee wa Moabu na Midiani wakapeleka zawadi za uaguzi, wakaondoka kwenda kwa Balamu. Walifika, wakamupa Balamu ujumbe wa Balaki.


Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende kule ngambo kukutana na Yawe.


Nimepewa amri ya kubariki, naye amebariki wala siwezi kuigeuza.


Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo, wala uchawi juu ya watu wa Israeli. Sasa juu ya Israeli, watu watasema: Muangalie maajabu Mungu aliyotenda!


Basi, Balaki akamupeleka Balamu mpaka kwenye kilele cha mulima Peori, ambapo mutu akisimama anaona katika jangwa.


Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.


Balaki akafanya kama vile alivyoambiwa na Balamu, kisha akatoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Mukumbuke kwamba wanawake ndio waliofuata shauri la Balamu, wakasababisha Waisraeli wamwasi Yawe kule Peori hata ugonjwa mukali ukawafikia watu wa Yawe.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Mutu akimukamata adui yake atamwacha aende salama? Kwa lile ulilonitendea, Yawe akupe zawadi njema!


Mara moja, Saulo alikwenda kwenye jangwa la Zifu kumutafuta Daudi akiwa na waaskari waliochaguliwa elfu tatu wa Israeli.


Saulo akamwambia Daudi: “Mungu akubariki mwana wangu Daudi. Utafanya mambo makubwa, nawe utafanikiwa katika yote.” Basi, Daudi akaenda zake; Saulo naye akarudi kwake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ