Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 23:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Balamu akamutolea Balaki mashairi yake, akasema: Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, hakika, mufalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki: Kuja uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, hakika, kuja uwakaripie Waisraeli!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 23:7
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wana wa Semu walikuwa Elamu, Asuri, Aripakisadi, Ludi na Aramu.


Kwenda Padani-Aramu, kwa nyumba ya babu yako Betueli, uoe mumoja kati ya wabinti za mujomba wako Labani.


Akatambua vilevile kwamba Yakobo alimutii mama yake na baba yake, akakwenda Padani-Aramu.


Alipowachekelea Waisraeli, Yonatani mwana wa Simei, ndugu ya Daudi, alimwua.


Halafu aliyefuata kati ya wale mashujaa watatu alikuwa Eleazari mwana wa Dodayi, wa ukoo wa Muahoa. Siku moja, Eleazari alikuwa pamoja na Daudi walipowatukana Wafilistini waliokuwa wamekusanyika kwa kupigana vita. Waisraeli waliwakimbia Wafilistini.


Yobu akaendelea kutoa masemi yake, akasema:


Kisha Yobu akaendelea na masemi yake, akasema:


Ninatega sikio, nisikilize mezali, ninafafanua kitendawili kwa muziki wa zeze.


Nitasema nanyi kwa mafumbo, nitasema mambo yaliyofichwa tangu zamani;


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Wewe mwanadamu! Tega kitendawili, uwaambie Waisraeli fumbo.


Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo, watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema: Tumeangamia kabisa; amekamata inchi yetu, ameiondoa katika mikono yetu. Mashamba yetu ameyagawanya kwa wale waliotuteka.


Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo na kumutungia misemo ya kitambi: Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako, na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi! Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?


kuna watu wa taifa fulani waliotoka Misri, nao wameenea kila pahali katika inchi. Ameniomba niende kuwalaani watu hao kusudi pengine ataweza kupigana nao na kuwafukuza.


Nitakupatia heshima kubwa, na chochote utakachoniomba nitakutimizia. Kuja uwalaani watu hawa.


Halafu, Balamu akamutolea Balaki mashairi yake: Simama, Balaki, usikie! Unisikilize, ewe mwana wa Sipori!


Balamu akarudi, akamukuta Balaki akisimama palepale karibu na sadaka yake ya kuteketezwa kwa moto, pamoja na wakubwa wote wa Moabu.


Basi, Balamu akasema mashairi haya: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Beori, mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho,


Kisha Balamu akawaangalia Wakeni, akatoa mashairi haya: Makao yenu ni salama, enyi Wakeni, kama chicha juu kabisa ya mulima.


Tena Balamu akatoa mashairi haya: Ole! Nani ataishi Mungu atakapofanya hayo?


naye akasema mashairi haya ya Yawe: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Peori mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho.


Yesu akawaambia tena mufano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni unafanana na chachu mwanamuke mumoja aliyoitwaa na kuichanga na vipimo vitatu vya unga kwa kuponda mikate hata yote ikapata kuvimba.”


Ilitokea vile kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii: “Nitasema nao kwa mifano, nitawaambia maneno yaliyofichwa tangu kuumbwa kwa dunia.”


Basi hao wakubwa wakatafuta kumukamata Yesu, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao. Lakini kwa sababu waliogopa kundi la watu, wakamwacha ajiendee.


“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,


Kisha Mufilistini yule aliendelea kusema kwa majivuno: “Ninawataka waaskari wa Waisraeli siku hii kumutoa mutu mumoja akuje kupigana nami.”


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Lakini Daudi akamwambia Goliati: “Wewe unanifikia kwa upanga na mikuki. Lakini mimi ninakufikia kwa jina la Yawe wa majeshi, Mungu wa waaskari wa Israeli, ambaye wewe umemutukana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ