Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 23:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 23:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Abrahamu akainua macho, akaona kondoo dume, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi, akakwenda, akamutwaa yule kondoo, akamutoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto pahali pa mwana wake.


Mungu akamwambia: “Umutwae mwana wako, Isaka, mwana wako wa pekee unayemupenda, uende mpaka inchi ya Moria, umutoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mulima nitakaokuonyesha.”


Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.


Halafu Yetro, baba mukwe wa Musa, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Naye Haruni akakuja pamoja na wazee wa Israeli kwa kula chakula pamoja na Yetro, mbele ya Yawe.


Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:


Balamu akamwambia Balaki: Hainipasi tu kusema maneno Yawe aliyoweka ndani ya kinywa changu?


Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende kule ngambo kukutana na Yawe.


Balaki akafanya kama vile Balamu alivyosema. Basi, wakatolea juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Lakini Balamu akamujibu Balaki: Sikukuambia kwamba kile Yawe anachosema ndicho ninachopaswa kufanya?


Mungu akakutana naye. Balamu akamwambia: Nimetayarisha mazabahu saba na kutoa ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja juu ya kila mazabahu.


Sasa Balamu akatambua kwamba Yawe alipenda kuwabariki Waisraeli, kwa hiyo hakukwenda sawa vile mara ingine kwa kutafuta uchawi. Akaelekea kwenye jangwa,


Shetani akamupeleka tena mpaka juu ya mulima murefu, akamwonyesha falme zote za dunia na utajiri wao.


Lakini mimi sikumusikiliza Balama, naye akawabariki, nami nikawaokoa ninyi toka mikono ya Balaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ