Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 23:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Balamu akamwambia Balaki: Unijengee mazabahu saba hapa kisha uniletee ngombe dume saba na kondoo dume saba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 23:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hata kama mukiniambia: ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


Wakamutolea Mungu sadaka: ngombe dume saba na kondoo dume saba kwa sababu aliwasaidia wale Walawi waliolibeba Sanduku la Agano la Yawe.


Wakaleta ngombe dume saba, kondoo dume saba, wana-kondoo saba na mbuzi dume saba, kuwa sadaka ya maondoleo ya zambi, kwa ajili ya jamaa ya kifalme, ya Pahali Patakatifu na ya watu wa Yuda. Kwa hiyo, mufalme akawaambia makuhani waliokuwa wazao wa Haruni wawateketeze juu ya mazabahu ya Yawe.


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Kila siku, katika muda huo wa siku saba, atamutolea Yawe sadaka ya ngombe dume saba na kondoo dume saba wasiokuwa na kilema kwa kuwateketeza kwa moto. Tena ni lazima atoe sadaka kila siku kuwa sadaka ya kusamehewa zambi.


Kesho yake, Balaki akamutwaa Balamu, akapanda naye mpaka Bamoti-Bali; kutoka huko, Balamu aliweza kuwaona wamoja kati ya Waisraeli.


Balaki akafanya kama vile Balamu alivyosema. Basi, wakatolea juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Balamu akamwambia Balaki: Unijengee mazabahu saba hapa, unitayarishie ngombe dume saba na kondoo dume saba.


Balaki akafanya kama vile alivyoambiwa na Balamu, kisha akatoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Siku ya saba mutatoa ngombe dume saba, kondoo dume watatu, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ