Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Balamu akawaambia: Mulale huku usiku huu, nami nitawajulisha vile Yawe atakayoniambia. Basi, wazee hao wa Moabu wakakaa na Balamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:8
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mutu wa Mungu akamwambia: “Hata kama ukinipa nusu ya urizi wako, sitakwenda pamoja nawe. Sitakula wala kunywa maji pahali hapa,


Lakini Mikaya akamujibu: “Kama vile Yawe anavyoishi, mimi nitasema tu yale Yawe atakayoniambia.”


Umewapanda nao wameota mizizi, wanastawi na kuzaa matunda. Wanakujua kwa midomo tu, lakini mioyo yao iko mbali nawe.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.


Lakini Balamu akawajibu watumishi wa Balaki: Hata kama Balaki atanipa nyumba yake imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kuvunja amri ya Yawe, Mungu wangu, juu ya jambo lolote, dogo au kubwa.


Balamu akamujibu Balaki: Sasa nimekuja! Lakini, nina mamlaka ya kusema neno lolote? Jambo Mungu atakaloniambia ndilo ninalopaswa kusema.


Basi, wazee wa Moabu na Midiani wakapeleka zawadi za uaguzi, wakaondoka kwenda kwa Balamu. Walifika, wakamupa Balamu ujumbe wa Balaki.


Kisha Mungu alimufikia Balamu, akamwuliza: Ni nani hawa wanaokaa nawe?


Balamu akamwambia Balaki: Hainipasi tu kusema maneno Yawe aliyoweka ndani ya kinywa changu?


Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.


Niliwaambia kwamba hata kama ungenipa nyumba yako imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kubadilisha agizo la Yawe, kwa kufanya jambo lolote, jema au baya kwa mapenzi yangu mwenyewe. Nilisema kwamba atakachosema Yawe ndicho nitakachosema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ