Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kuja sasa uwalaani watu hawa kwa ajili yangu maana wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwashinda na kuwafukuza wasiingie katika inchi yangu, kwa maana unajua kwamba wewe ukimubariki mutu anabarikiwa, ukimulaani mutu analaaniwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:6
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.”


Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Wakati ule, yule mutumishi aliyetumwa kwenda kwa Mikaya, akamwambia: “Manabii wengine wote kwa pamoja, wamemutabiria mufalme ushindi. Tafazali, nawe vilevile ufanye kama wao, umutabirie mazuri.”


Basi, Ahabu akakusanya manabii yapata mia ine, akawauliza: “Niende au nisiende kushambulia Ramoti-Gileadi?” Nao wakamujibu: “Kwenda! Yawe atakupatia ushindi.”


Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwomba shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye, hatabiri jambo zuri juu yangu hata kidogo, lakini baya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”


Kwa sababu watu wa Israeli, walipokuwa wanasafiri toka Misri, wao hawakuwapa chakula wala maji ya kunywa, pahali pake wakamulipa Balamu kwa kuwalaani watu wa Israeli, lakini Mungu wetu akageuza laana yao kuwa baraka.


Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Maono yao ni ya uongo mutupu na wanachotabiri ni udanganyifu mutupu. Wanasema “Ni ujumbe wa Yawe” lakini Yawe hakuwatuma; kisha wanamutazamia atimize yale wanayosema.


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


Mungu akamwambia Balamu: Usiende pamoja na watu hawa, wala usiwalaani watu hao maana wamebarikiwa.


Nitakupatia heshima kubwa, na chochote utakachoniomba nitakutimizia. Kuja uwalaani watu hawa.


Kisha, Balaki akamwambia Balamu: Tuende pahali pengine ambapo utaweza kuwaona; hata hivyo utaona tu sehemu yao, hautaweza kuwaona wote. Kisha uwalaani kutoka huko kwa ajili yangu.


Balaki akamwambia Balamu: Kuja, nitakupeleka pahali pengine. Labda Mungu atakubali uwalaani watu hao kutoka huko kwa ajili yangu.


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Siku moja tulipokuwa tukienda kule kwenye nafasi ya kufanyia maombi, tukakutana na mujakazi mumoja. Yule mwanamuke alikuwa na pepo wa kuaguza ndani yake. Na kwa njia ya uaguzi ule aliwatajirisha wabwana wake.


“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,


Naye Balaka mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, akakuja na kuwashambulia Waisraeli. Akamwalika Balama mwana wa Beori akuje kuwalaani ninyi.


Goliati akamwuliza Daudi: “Sasa, hiyo fimbo ni ya nini? Unazani mimi ni imbwa hata unifikie kwa fimbo?” Mufilistini yule akamulaani Daudi kwa miungu yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ