Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 akapeleka ujumbe kwa Balamu mwana wa Beori, huko Petori, karibu na muto Furati katika inchi ya Amawi. Akamwambia Balamu hivi: Kuna taifa ambalo limetoka Misri, nalo limeenea kila pahali katika inchi, tena linatishia kutwaa inchi yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:5
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Yawe akawafanya watu wake wazae sana; akawajalia nguvu kuliko waadui zao.


Walifunika inchi yote ya Misri, hata inchi ikaonekana kuwa giza. Walikula mimea yote na matunda yote yaliyobaki wakati wa ile mvua ya mawe. Hakuna hata jani moja lililobakia katika inchi. Hakuna jani lolote lililobakia juu ya miti wala mimea popote katika inchi yote ya Misri.


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


Balamu akamutolea Balaki mashairi yake, akasema: Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, hakika, mufalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki: Kuja uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, hakika, kuja uwakaripie Waisraeli!


Kati ya watu hao waliouawa, kulikuwa wafalme watano wa Midiani: Ewi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile wakamwua Balamu mwana wa Beori.


“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,


kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.


Balamu mwaguzi mwana wa Beori ambaye Waisraeli walimwua alikuwa mumoja wao.


Naye Balaka mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, akakuja na kuwashambulia Waisraeli. Akamwalika Balama mwana wa Beori akuje kuwalaani ninyi.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ