Hesabu 22:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
36 Balaki alipopata habari kwamba Balamu anakuja, akatoka kwenda kumupokea katika muji wa Ari, muji uliokuwa kwenye ukingo wa muto Arnoni kwenye mupaka wa Moabu.
Abramu aliporudi kisha kumushinda mufalme Kedorilaomeri na wenzake, mufalme wa Sodoma akatoka na kwenda kukutana naye katika bonde la Sawe ni kusema bonde la Mufalme.
Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima
Yosefu akapanda gari lake la farasi, akakwenda kumupokea baba yake Israeli, kule Goseni. Alipomufikia baba yake, alimukumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.
Lakini malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Kwenda na watu hawa, lakini utasema tu kile nitakachokuambia. Basi, Balamu akaendelea na safari pamoja na viongozi wa Balaki.
Wandugu waamini wa Roma waliposikia habari zetu wakakuja kutuona kwenye Soko la Apio na wengine kwenye Tiretaberne. Paulo alipowaona, akamushukuru Mungu na kutiwa tena moyo.
“Kisha Yawe akatuamuru: ‘Basi! Muanze safari. Muvuke bonde la Arnoni. Mimi nimetia katika mikono yenu Sihoni, mufalme wa Waamori wa Hesiboni na inchi yake. Mushambulie na kuanza kurizi inchi yake.
Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.