Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Hapo, Yawe akafungua macho ya Balamu, naye akamwona malaika wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa toka kifuko chake. Balamu akajitupa uso mpaka chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:31
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamufumbua Hagari macho, naye akaona kisima cha maji. Akakwenda akajaza chupa maji, akamukunywesha mutoto wake.


Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Ee Yawe, simama sasa mwanadamu asishinde! Uyakusanye sasa hivi mataifa mbele yako, uyahukumu.


Musa akainama uso mpaka chini haraka, akamwabudu Mungu.


Punda akamwambia Balamu: Mimi si yuleyule punda wako aliyekubeba maisha yako yote mpaka siku hii ya leo? Nimekwisha kukutendea namna hii? Balamu akajibu: Hapana.


mashairi ya mutu aliyesikia maneno ya Mungu, na mutu anayejua maarifa ya Mungu Mukubwa, mutu anayeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini, macho wazi.


Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu, mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.


Halafu, macho yao yakafumbuliwa, wakamutambua. Lakini yeye akatoweka, nao hawakumwona tena.


Yesu alipowaambia: “Ni mimi,” wakarudi nyuma na kuanguka.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Naye akamujibu: “Wala wenu wala wa waadui zenu! Lakini mimi ni jemadari wa jeshi la Yawe, na sasa nimefika.” Yoshua akainama chini kwa heshima, kisha akamwuliza: “Bwana wangu, unataka mimi mutumishi wako nifanye nini?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ