Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Basi, punda akamwona malaika huyo wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa. Kwa hiyo akaacha njia, akaenda pembeni. Balamu akamupiga huyo punda, akamurudisha katika njia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:23
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Elisha akaomba: “Ee Yawe, umufumbue macho kusudi apate kuona!” Basi, Yawe akamufumbua macho yule kijana, akaona farasi na magari ya moto yakiwa kila pahali katika mulima wote, kumuzunguka Elisha.


Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Hata korongo anajua wakati wa kuhama; njiwa, mbaruwayi na koikoi, wanajua nyakati zao za kurudi. Lakini hawa watu wangu hawajui maagizo ya Yawe.


Mimi Danieli peke yangu niliona maono hayo. Wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini walishikwa na hofu sana, wakakimbia, wakajificha.


Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu Balamu alikuwa anakwenda; hivyo malaika wa Yawe akakutana naye katika njia. Wakati huo Balamu alikuwa amepanda juu ya punda wake naye alisindikizwa na watumishi wake wawili.


Kisha malaika huyo wa Yawe akatangulia mbele, akasimama pahali hiyo njia ilikuwa nyembamba, kati ya mashamba ya mizabibu na kuta pande zote mbili.


Watu waliokuwa pamoja nami wakaona mwangaza ule, lakini hawakusikia sauti ya yule aliyekuwa akinisemesha.


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


lakini alikaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Basi punda, ambaye hasemi, alisema kama mutu na kuzuiza kitendo cha upumbafu wa yule nabii.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ