Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Basi, Mungu akamufikia Balamu usiku ule, akamwambia: Kama watu hawa wamekuja kukuita, kwenda pamoja nao, lakini fanya tu kile nitakachokuambia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:20
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.


Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.


Lakini Yawe akaniambia: Usiseme kwamba ungali kijana. Utakwenda kwa watu ninaokutuma kwao, na maneno yote nitakayokuamuru, utayasema.


Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme, kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.


Lakini tafazali mulale hapa usiku huu kama wale wenzenu, nami nipate kujua kile Yawe atakachoniambia tena.


Lakini malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Kwenda na watu hawa, lakini utasema tu kile nitakachokuambia. Basi, Balamu akaendelea na safari pamoja na viongozi wa Balaki.


Balamu akamwambia Balaki: Hainipasi tu kusema maneno Yawe aliyoweka ndani ya kinywa changu?


Yawe akakutana na Balamu, akamupa maneno atakayosema, na kumwambia arudi kwa Balaki.


Lakini Balamu akamujibu Balaki: Sikukuambia kwamba kile Yawe anachosema ndicho ninachopaswa kufanya?


Yawe akamupa Balamu maneno atakayosema na kumwambia arudi kwa Balaki.


Niliwaambia kwamba hata kama ungenipa nyumba yako imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kubadilisha agizo la Yawe, kwa kufanya jambo lolote, jema au baya kwa mapenzi yangu mwenyewe. Nilisema kwamba atakachosema Yawe ndicho nitakachosema.


Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu, mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ