Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mungu akamwambia Balamu: Usiende pamoja na watu hawa, wala usiwalaani watu hao maana wamebarikiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:12
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”


Heri taifa ambalo limejaliwa hayo! Heri taifa ambalo Yawe ndiye Mungu wao!


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


kuna watu wa taifa fulani waliotoka Misri, nao wameenea kila pahali katika inchi. Ameniomba niende kuwalaani watu hao kusudi pengine ataweza kupigana nao na kuwafukuza.


Basi, asubui yake Balamu akaamuka, akawaambia wazee wa Balaki: Murudie katika inchi yenu, kwa maana Yawe hapendi kuniruhusu kwenda pamoja nanyi.


Kuja sasa uwalaani watu hawa kwa ajili yangu maana wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwashinda na kuwafukuza wasiingie katika inchi yangu, kwa maana unajua kwamba wewe ukimubariki mutu anabarikiwa, ukimulaani mutu analaaniwa.


Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo, wala uchawi juu ya watu wa Israeli. Sasa juu ya Israeli, watu watasema: Muangalie maajabu Mungu aliyotenda!


Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.


Nitamulaani namna gani mutu ambaye Mungu hakumulaani? Nitawakaripia watu ambao Yawe hakuwakaripia?


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”


Kwa maana Mungu habadilishi mafikiri juu ya zawadi anazotoa, wala juu ya wale anaowachagua.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.


Mutabarikiwa munaporudi kwa nyumba na munapotoka inje.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


Mutabarikiwa kuliko watu wengine wote katika ulimwengu. Kati yenu hakutakuwa mwanaume wala mwanamuke tasa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ