Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 22:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Waisraeli wakaanza safari tena, wakaenda kupiga kambi yao katika bonde za Moabu, upande wa mashariki wa muto Yordani, kuelekea muji wa Yeriko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 22:1
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,


na kutoka Bamoti mpaka kwenye bonde linaloingia katika inchi ya Moabu, kwenye kilele cha mulima Pisiga, kinachoelekea chini katika jangwa.


Musa na kuhani Eleazari wakazungumuza na watu kwenye inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya muto Yordani, karibu na Yeriko, wakawaambia:


wakamupelekea Musa na Eleazari, na Waisraeli wote waliokuwa katika kambi katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya Yordani karibu na Yeriko.


Hatutarizi mali yoyote kati yao ngambo ya muto Yordani, kwa sababu sisi tumepata maeneo yetu ngambo hii, upande wa mashariki wa muto Yordani.


Makabila hayo mawili na nusu yamepata urizi wao ngambo ya muto Yordani upande wa mashariki, kuelekea Yeriko, jua linakotokea.


Yawe akasema na Musa katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na Yeriko, akamwambia:


Hizo ndizo amri na maagizo ambayo Yawe aliwapa Waisraeli kwa njia ya Musa katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na muji wa Yeriko.


Musa akaanza kuwaelezea watu sheria ya Mungu wakati walipokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani. Akawaambia hivi:


“Wakati huo tukatwaa inchi hiyo ya wale wafalme wawili wa Waamori waliokuwa wanakaa ngambo ya muto Yordani, katikati ya muto Arnoni na mulima Hermoni.


Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,


Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.


maji yaliyokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yalisimama na kulundikana mpaka kule Adamu kijiji kinachokuwa karibu na muji wa Zaretani. Maji yaliyokuwa yanateremuka kwenda katika bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, yalitoweka kabisa, watu wakavuka mbele ya Yeriko.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ