Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,
Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,
Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.
maji yaliyokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yalisimama na kulundikana mpaka kule Adamu kijiji kinachokuwa karibu na muji wa Zaretani. Maji yaliyokuwa yanateremuka kwenda katika bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, yalitoweka kabisa, watu wakavuka mbele ya Yeriko.