Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 21:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Waisraeli wakafunga safari kutoka mulima Hori, wakapitia njia inayoelekea bahari Nyekundu kusudi wazunguke inchi ya Edomu. Lakini katika njia watu wakavunjika moyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 21:4
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tutashambulia kutokea upande gani?” Yoramu akajibu: “Tutashambulia kutokea jangwa la Edomu.”


Musa akawaelezea Waisraeli maneno hayo. Lakini wao hawakumusikiliza kwa sababu walikuwa wamekufa moyo kutokana na utumwa mukali.


Kwa sababu Waamaleki na Wakanana wanakaa katika mabonde ya inchi hiyo, kesho mugeuke nyuma muende katika jangwa kuelekea bahari ya Shamu.


Musa akafanya kama vile alivyoamriwa na Yawe. Wote watatu wakapanda juu ya mulima mbele ya watu wote wengine.


Mbona munawavunja moyo Waisraeli wasiende katika inchi ambayo Yawe amewapa?


Wao walikwenda mpaka bonde la Eskoli, wakaiona inchi, lakini waliporudi, wakavunja Waisraeli moyo kusudi wasiingie katika inchi Yawe aliyowapa.


Kutoka mulima Hori, Waisraeli wakapiga kambi yao Salmona.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Lakini ninyi, mugeuke na kurudi katika jangwa kuelekea bahari Nyekundu.’


“Kisha, tukageuka, tukasafiri katika jangwa kwa kupitia njia ya bahari Nyekundu, kama vile Yawe alivyoniambia. Tukatangatanga karibu na mulima Seiri kwa muda murefu.


Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ