Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 21:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kutoka huko wakasafiri, wakapiga kambi upande wa kaskazini wa muto Arnoni, ambao unatiririka kutoka katika inchi ya Waamori na kupitia katika jangwa. Muto Arnoni ulikuwa mupaka kati ya Wamoabu na Waamori.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 21:13
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka, wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao, ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.


Moabu imepatishwa haya maana imevunjika. Muomboleze na kuililia. Mutangaze kandokando ya muto Arnoni, kwamba Moabu imeharibika kabisa.


Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita za Yawe: “Muji wa Wahebu katika inchi ya Sufa, na mabonde ya Arnoni,


Balaki alipopata habari kwamba Balamu anakuja, akatoka kwenda kumupokea katika muji wa Ari, muji uliokuwa kwenye ukingo wa muto Arnoni kwenye mupaka wa Moabu.


“Yawe akatuambia: ‘Muondoke sasa, muvuke kijito Zeredi’. Basi, tukavuka kijito Zeredi.


‘Leo hii mutauvuka mupaka wa Moabu kwa kupitia inchi ya Ari.


“Kisha Yawe akatuamuru: ‘Basi! Muanze safari. Muvuke bonde la Arnoni. Mimi nimetia katika mikono yenu Sihoni, mufalme wa Waamori wa Hesiboni na inchi yake. Mushambulie na kuanza kurizi inchi yake.


Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ