Upande wa kusini, toka Tamari mupaka utaendelea mpaka kwenye chemichemi ya Meriba-Kadesi. Kutoka Meriba-Kadesi mupaka utaelekea kusini magaribi mpaka bahari ya Mediteranea ukipitia upande wa mashariki ya inchi ya Misri.
Eneo linalopakana na kabila la Gadi kuelekea kusini, mupaka utatoka muji wa Tamari mpaka kwenye chemichemi za Meriba-Kadesi na kupitia upande wa mashariki ya Misri mpaka kwenye bahari ya Mediteranea.
Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.
Waisraeli wakafunga safari kutoka mulima Hori, wakapitia njia inayoelekea bahari Nyekundu kusudi wazunguke inchi ya Edomu. Lakini katika njia watu wakavunjika moyo.