Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.
Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa mufalme wa Edomu wakimwomba awaruhusu kupita katika inchi yake, lakini mufalme wa Edomu akakataa. Basi wakamwomba mufalme wa Moabu ruhusa naye vilevile akakataa. Kwa hiyo Waisraeli wakabaki Kadesi.
Lakini Sihoni hakuwakubali Waisraeli wapite katika inchi yake. Basi, Sihoni akakusanya watu wake wote, akapiga kambi kule Yahasa, akawashambulia Waisraeli.