Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 20:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Tukamulilia Yawe, naye akasikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri. Sasa tuko hapa Kadesi, muji unaopakana na inchi yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 20:16
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waisraeli walipoinua macho na kumwona mufalme wa Misri akikuja na jeshi lake nyuma yao, wakashikwa na hofu kubwa, wakamulilia Yawe.


Basi, malaika wa Mungu aliyekuwa mbele ya kundi la Waisraeli akaondoka akakaa nyuma yao. Na ule munara wa wingu vilevile ukaondoka mbele ukasimama nyuma yao.


Muangalie, mimi ninamutuma malaika awatangulie katika safari kusudi awalinde na kuwafikisha katika inchi niliyowatayarishia.


Nitamutuma malaika awaongoze. Nitawafukuza Wakanana, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wamelazimishwa kufanya kazi za kitumwa na Wamisri, nikalikumbuka agano langu.


Danieli akamujibu mufalme: Uishi milele, ee mufalme!


Jinsi babu zetu walivyokwenda Misri, ambako tuliishi kwa muda murefu na jinsi Wamisri walivyowatesa babu zetu, wakatutesa na sisi vilevile.


Uturuhusu tupite katika inchi yako; hatutakwenda pembeni na kuingia katika mashamba au katika mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visima vyenu; tutapita moja kwa moja katika barabara kubwa ya mufalme mpaka tutakapoondoka katika inchi yako.


Kutoka Kadesi, wakapiga kambi yao juu ya mulima Hori, kwenye mupaka wa inchi ya Edomu.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Kwa kuwa aliwapenda wazee wenu, yeye amewachagua ninyi wazao wao, akawatoa yeye mwenyewe katika inchi ya Misri kwa nguvu yake kubwa.


Eneo la inchi watu wa kabila la Yuda walilopewa kwa kura kulingana na jamaa zake lilienea tangu kusini mashariki mpaka kwa mupaka wa Edomu. Sehemu ya kusini kabisa ilikuwa jangwa la Sini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ