Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”
Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.
Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.
kwa sababu ninyi wote wawili mulivunja uaminifu wenu kwangu mbele ya Waisraeli mulipokuwa kwenye maji ya Meriba, karibu na muji wa Kadesi, katika jangwa la Sini. Mukakosa kuhakikisha utakatifu wangu kati ya Waisraeli.
Juu ya kabila la Lawi, akasema: “Ee Yawe, upatie wazao wa Lawi shauri lako, shauri lako kwa hao waaminifu wako, ambao uliwajaribu huko Masa. Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.