Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 20:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini Yawe akamwambia Musa na Haruni: Kwa sababu ninyi hamukuniamini mimi, wala kuniheshimu mbele ya macho ya Waisraeli, basi kwa sababu hiyo hamutaingiza watu hawa katika ile inchi niliyowapa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 20:12
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”


Walimukasirikisha Mungu penye maji ya Meriba. Musa akapata taabu kwa ajili yao.


Ee Yawe, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza; ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliwaazibu kwa makosa yao.


Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu.


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile, utaanza kuwaza ndani ya moyo wako na kupanga mipango miovu na kusema:


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Ikiwa hivi ndivyo utakavyonitendea, afazali uniue mara moja! Kama ninapata kukubaliwa mbele yako, usiniache kuendelea katika taabu yangu.


Haruni atakufa; hataingia katika inchi ambayo nimewapa Waisraeli kwa sababu ninyi wawili muliasi amri yangu kule Meriba.


kwa sababu hamukuitii amri yangu kule katika jangwa la Sini, wakati watu wote pamoja waliponigombanisha kule Meriba. Ninyi hamukuacha utukufu wangu uonekane mbele yao walipotaka wapewe maji. (Meriba ni chemichemi ya maji ya Kadesi katika jangwa la Sini).


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [


Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”


Heri kwako wewe uliyesadiki kwamba maneno yale uliyoambiwa kutoka kwa Bwana yatatimizwa!”


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Hakuona shaka juu ya ahadi aliyopewa na Mungu wala kupoteza tumaini, lakini imani yake ilimutia nguvu hata akamutukuza Mungu.


Yawe akanikasirikia mimi vilevile kwa sababu yenu, akasema: ‘Hata wewe Musa hautaingia katika inchi hiyo.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”


Kwa sababu yenu Yawe, Mungu wenu, alinikasirikia, akaapa kwamba mimi sitavuka muto Yordani kuingia katika inchi ile nzuri anayowapa ikuwe mali yenu.


“Mutumishi wangu Musa amekufa, sasa muvuke muto Yordani, wewe pamoja na Waisraeli wote mpaka kwenye inchi ile ambayo ninawapa.


Lakini mumutukuze Bwana wenu Kristo ndani ya mioyo yenu. Mukuwe tayari wakati wowote kumujibu kila mutu anayewauliza juu ya tumaini munalokuwa nalo. Lakini mufanye vile kwa upole na heshima,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ