Nyama wote wanaotembelea kwa vitanga vyao ingawa wana miguu mine, ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa muzoga wa nyama kama huyo atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Ikiwa muzoga wa viumbe hao unaangukia kitu chochote, kikuwe ni kifaa cha mbao au nguo au ngozi au gunia au chombo chochote kinachotumiwa kwa kazi yoyote, chombo hicho kitakuwa kichafu mpaka magaribi. Kwa kukifanya kikuwe safi kinapaswa kusafishwa kwa maji.
Mutu yeyote akikula nyama ya muzoga huo atafua nguo yake na atakuwa muchafu mpaka magaribi. Na yeyote atakayebeba muzoga huo, atafua nguo zake, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Mutu atakayezoa majivu ya ngombe huyo anapaswa kufua nguo zake, lakini atakuwa muchafu mpaka magaribi. Sharti hili ni la kufuata siku zote kwa Waisraeli na watu wengine watakaoishi pamoja nao.
Katika siku ya tatu na ya saba, mutu anayekuwa safi atamunyunyizia mutu anayekuwa muchafu maji hayo; hivyo katika siku ya saba, atamutakasa mutu huyo anayekuwa muchafu, naye atafua nguo zake na kuoga, na magaribi atakuwa safi.
Kuhani Mukubwa anapeleka damu ya nyama ndani ya Pahali Patakatifu Sana kwa ajili ya kuitoa kuwa sadaka ya kusamehewa zambi lakini viungo vyote vya nyama wale vinateketezwa kwa moto mbali na kambi.