Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 19:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Mutu anayekuwa safi atatwaa hisopo, halafu ataichovya katika maji hayo, kisha atainyunyizia hema, vyombo vyote vinavyokuwa ndani ya hema na watu wanaokuwa ndani. Atamunyunyizia vilevile mutu aliyegusa mufupa wa mutu, au mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida, au aliyegusa kaburi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 19:18
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.


Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Kwa ajili ya wale waliojichafua, watatwaa majivu ya sadaka ya zambi iliyoteketezwa, majivu hayo yatachanganywa na maji ya muto.


Katika siku ya tatu na ya saba, mutu anayekuwa safi atamunyunyizia mutu anayekuwa muchafu maji hayo; hivyo katika siku ya saba, atamutakasa mutu huyo anayekuwa muchafu, naye atafua nguo zake na kuoga, na magaribi atakuwa safi.


Mutu anayekuwa safi atazoa majivu ya ngombe huyo na kuyapeleka pahali safi inje ya kambi. Yatalindwa na kutumiwa na jamii nzima ya Israeli kwa kutengeneza maji ya utakaso kwa kuondoa zambi.


Uwatakase wapate kujitoa kwako kabisa kwa njia ya ukweli, maana yake kwa njia ya neno lako la kweli.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Kwa maana, kwanza Musa aliwatangazia watu wote amri zote za Sheria. Kisha akatwaa damu ya ngombe pamoja na maji, naye akavinyunyiza juu ya kitabu cha Sheria na juu ya watu wote akitumia manyoya mekundu na vitawi vya muti wa hisopo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ