Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 19:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Anayegusa maiti, ni kusema mwili wa mutu aliyekufa, asipojitakasa, anachafua hema la Yawe, naye atatengwa na watu wa Israeli. Mutu huyo atabaki muchafu kwa sababu hakunyunyiziwa yale maji ya utakaso.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 19:13
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumupakaa mutu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mutu huyu atatengwa mbali na watu wake.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Mumoja wao akijichafua, atakaa na hali hiyo kwa muda wa siku saba. Kisha atakuwa safi.


Ndivyo mutakavyotenga Waisraeli na uchafu wao, kusudi wasikufe katika uchafu wao juu ya kuchafua hema langu linalokuwa kati yao.


Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.


Uwaambie hivi: Kama mumoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote akikaribia vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wamevitakasa kwa ajili yangu mimi Yawe akiwa muchafu, mutu huyu atatengwa nami. Mimi ni Yawe.


Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,


Mutu yeyote akitenda zambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Yawe, yeye ana kosa, na atalipa azabu ya kosa lake.


Au mutu akigusa kitu chochote toka kwa mwanadamu kinachohesabiwa kuwa kichafu, kikuwe kile ambacho kinamufanya mutu kuwa muchafu bila kujua, basi, atakapojua atakuwa na kosa.


na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


iliyotolewa sadaka ya amani kwa Yawe. Lakini mutu yeyote anayehesabiwa kuwa muchafu akikula nyama hiyo, atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.


Lakini mutu yeyote atakayekosa kwa makusudi, akuwe mwanainchi au mugeni, atakuwa amemutukana Yawe, na anapaswa kutengwa mbali kati ya watu wake.


Na hii ndiyo sheria ya kufuatwa kama mutu akikufia ndani ya hema: Kila mutu atakayeingia ndani ya hema hilo, au aliyekuwa ndani ya hema hilo, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Mutu anayekuwa safi atatwaa hisopo, halafu ataichovya katika maji hayo, kisha atainyunyizia hema, vyombo vyote vinavyokuwa ndani ya hema na watu wanaokuwa ndani. Atamunyunyizia vilevile mutu aliyegusa mufupa wa mutu, au mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida, au aliyegusa kaburi.


Katika siku ya tatu na ya saba, mutu anayekuwa safi atamunyunyizia mutu anayekuwa muchafu maji hayo; hivyo katika siku ya saba, atamutakasa mutu huyo anayekuwa muchafu, naye atafua nguo zake na kuoga, na magaribi atakuwa safi.


Lakini mutu muchafu asipojitakasa, mutu huyo atatengwa mbali na jamii, kwa sababu anachafua hema la Yawe. Kwa vile hakunyunyiziwa maji ya utakaso, yuko muchafu.


Mutu anayekuwa safi atazoa majivu ya ngombe huyo na kuyapeleka pahali safi inje ya kambi. Yatalindwa na kutumiwa na jamii nzima ya Israeli kwa kutengeneza maji ya utakaso kwa kuondoa zambi.


Hivi ndivyo utakavyowatakasa: uwanyunyizie maji ya utakaso kisha uwaambie wajinyoe mwili muzima, wafue nguo zao na kujitakasa.


Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.


Ni kwa sababu hii niliwaambia ninyi kama mutakufa katika zambi zenu. Musipoamini kwamba ‘Mimi Ndimi’, hakika mutakufa katika zambi zenu.”


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Mutu mubaya aendelee kufanya ubaya, na mutu muchafu azidi kuwa muchafu, na mutu mwema aendelee kutenda mema na mutu mutakatifu aendelee kuwa mutakatifu.”


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ