Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 19:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mutu akigusa maiti ya mutu yeyote, atakuwa muchafu kwa siku saba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 19:11
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Walitangatanga katika barabara kama vipofu, walikuwa wamejichafua kwa damu, hata mutu yeyote hangeweza kugusa nguo zao.


Kwa kuisafisha inchi, Waisraeli watatumia muda wa miezi saba kuzika maiti hizo.


Mumoja wao akijichafua, atakaa na hali hiyo kwa muda wa siku saba. Kisha atakuwa safi.


Hao wote ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Yawe akamwambia Musa: Uwaambie makuhani, wana wa Haruni, kwamba kusikuwe mutu yeyote kati yao atakayejichafua kwa kugusa maiti ya watu wa jamaa yake,


Asikaribie maiti wala kujichafua kwa maiti hata kama ni ya baba yake au ya mama yake.


Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,


Au kama mutu yeyote kati yenu akijichafua bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote kichafu, ikuwe ni muzoga wa nyama wa pori au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na kosa.


Hagai akawauliza tena: Mutu anayehesabiwa kuwa muchafu kwa kugusa maiti, akigusa sehemu ya vyakula hivi, chakula hicho kitakuwa kichafu? Makuhani wakamujibu: Ndiyo, kitakuwa kichafu.


Mutu yeyote akigusa mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida inje ya nyumba, au akigusa mufupa wa mutu au kaburi, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Wote wale wanaokuwa kati yenu ambao wameua mutu au kugusa maiti wanapaswa kukaa inje ya kambi kwa muda wa siku saba; mujitakase pamoja na mateka wenu katika siku ya tatu na ya saba.


Uwaamuru Waisraeli wamutoe inje ya kambi kila mutu mwenye ukoma, kila mutu anayetokwa usaha, na kila anayekuwa muchafu kwa kugusa maiti.


Siku zote atakazokuwa amejitakasa kwa Yawe, mutu huyo asikaribie maiti,


Mumoja wenu au mumoja wa wazao wenu akiwa muchafu kwa sababu amegusa maiti au akiwa mbali katika safari, lakini akiwa anataka kunifanyizia sikukuu ya Pasaka,


Lakini, watu wamoja waliokuwa pale walikuwa hawawezi kushiriki sikukuu hiyo ya Pasaka kwa sababu walikuwa wamegusa maiti, wakakuwa wachafu. Hao waliwaendea Musa na Haruni,


Halafu kesho yake Paulo akaenda na wale watu wane, na akajitakasa pamoja nao. Kisha akaingia ndani ya hekalu na kutangaza wakati siku za utakaso zitakapotimia, na sadaka itakayotolewa kama malipo kwa ajili ya kila mumoja wao.


Zile siku saba zilipokaribia kutimia, Wayuda wamoja waliotoka katika jimbo la Azia wakamwona Paulo ndani ya hekalu. Wao wakashawishi watu wote waliokusanyika, wakamukamata


Kwa njia ya mutu mumoja zambi iliingia katika dunia, nayo zambi ikaleta kifo. Ni hivi vilevile kifo kimefikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi.


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Zamani ninyi mulikuwa mumekufa kiroho kwa sababu ya makosa na zambi zenu.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ