Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kati ya vitu vitakatifu kabisa ambavyo haviteketezwi kwa moto, hivi vitakuwa vyenu: sadaka za vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka za kosa. Kila kitu watu watakachonitolea kama vile sadaka takatifu kitakuwa chako na wana wako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:9
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Feza zilizotolewa kwa sadaka za malipo kwa ajili ya kosa na kwa sadaka za usamehe wa zambi hazikuingizwa katika nyumba ya Yawe. Hizo zilikuwa ni mali ya makuhani.


Tunaahidi kuleta kila mwaka malimbuko yetu ya mazao na ya matunda ya kila muti kwenye nyumba ya Yawe.


Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.


Watakula sadaka ya vyakula, sadaka ya kusamehewa zambi, na sadaka ya malipo ya kosa. Kila kitu katika Israeli kilichotakaswa kwa Mungu kitakuwa chao.


Kwa nini hamukumukula katika Pahali Patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mulikuwa mumepewa huyo kwa kuondoa kosa ya Waisraeli wote pamoja na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe?


Kisha atachinja yule mwana-kondoo katika Pahali Patakatifu, wanapochinjia nyama wa sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka hii kwa ajili ya kosa na vilevile sadaka kwa ajili ya zambi, ni mali ya kuhani. Ni sadaka takatifu kabisa.


Sehemu inayobaki ya sadaka ya ngano, ni ya makuhani. Hiyo ni sehemu takatifu kabisa ya sadaka inayotolewa Yawe kwa moto.


Lakini kama kuhani amenunua mutumwa kwa kuwa mali yake, basi, yule mutumwa anaruhusiwa kula na vilevile wale waliozaliwa katika nyumba yake.


Jua litakapotua ndipo atakapokuwa safi. Nyuma ya pale ataweza kula vyakula vitakatifu maana hicho ndicho chakula chake.


Ikiwa mutawala ametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe, Mungu wake, na hivyo akakuwa na kosa,


Kama mutu wa kawaida ametenda zambi bila kukusudia, kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe na hivyo akakuwa na kosa,


Kama mutu yeyote akitakiwa kutoa ushuhuda kwenye baraza juu ya jambo aliloona au kusikia naye akikataa kusema kitu, basi, huo ni uovu na atabeba azabu ya zambi ile.


na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


Kuhani anayetolea sadaka hiyo ndiye atakayeikula. Itakuliwa katika Pahali Patakatifu, kwenye kiwanja cha hema la mukutano.


Hii ndiyo sheria ya ibada kuelekea sadaka kwa ajili ya kosa. Sadaka hiyo ni takatifu kabisa.


Wanaoruhusiwa kula sadaka hiyo ni wanaume wa ukoo wa makuhani peke yao; ni sadaka takatifu kabisa. Itakuliwa katika Pahali Patakatifu.


Sheria ni moja kuelekea sadaka kwa ajili ya kosa na sadaka kwa ajili ya zambi. Kuhani anayefanya ibada ya upatanisho ndiye atakayeitwaa.


Mutavikula vitu hivyo kama vitu vitakatifu kabisa, na ni wanaume tu ndio watakaovikula; vitu hivyo ni vitakatifu kwenu.


“Makuhani Walawi, ni kusema kabila lote la Lawi, wasikuwe na sehemu wala urizi katika Israeli. Wao watakula sehemu ya sadaka za Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ