Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:7
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Enyi wazao wa Haruni, mumutumainie Yawe; yeye ndiye musaada wenu na ngao yenu.


Nawe Musa umulete kwangu Haruni ndugu yako, pamoja na wana wake: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari. Utawachagua kati ya Waisraeli, kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Utawafunga mikaba katika viuno na kuwavalisha kofia zao. Hivi ndivyo utakavyowatakasa Haruni na wana wake kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani siku zote kwa ajili ya sharti la siku zote.


Lakini makuhani wa kabila la Lawi ambao ni wazao wa Zadoki walioendelesha kazi yangu katika pahali patakatifu pangu, wakati Waisraeli waliponiacha, hao ndio watakaoendelea kunitumikia na kuja mbele yangu kunitolea mafuta na damu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Hao tu ndio watakaoingia katika hekalu langu, nao watakaribia kwenye mazabahu kwa kunitumikia.


Kisha kutimiza kazi ya vitu vyangu vitakatifu, mumeruhusu watu wa mataifa mengine kutimiza kazi hiyo katika hekalu langu.


Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.


Hiyo ndiyo sehemu iliyotengwa kwa ajili ya Haruni na wana wake kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto, tangu siku walipowekwa kuwa makuhani wa Yawe.


Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.


Yawe akamwambia Haruni: Wewe hautakuwa na urizi wowote katika inchi yao, wala kuwa na fungu lako kati yao; mimi ni fungu lako na urizi wako kati ya Waisraeli.


Wao watafanya kazi utakazowapa na kutimiza mapaswa yao juu ya hema. Lakini hawana ruhusa ya kugusa vyombo vya hema, wala kukaribia mazabahu, kusudi wasikufe, nawe vilevile usikufe.


Utachagua Haruni na wana wake kusudi waweze kutimiza kazi zao za ukuhani; lakini kama mutu yeyote mwingine akikaribia, atauawa.


Musa na Haruni na wana wao watapiga kambi yao mbele ya hema takatifu upande wa mashariki, ni kusema mbele ya hema la mukutano kuelekea upande linakotokea jua. Kazi yao itakuwa kutumika kwenye Pahali Patakatifu kwa jambo lolote lililohitajika kufanyika kwa ajili ya Waisraeli. Mutu mwingine yeyote aliyesogea karibu alipaswa kuuawa.


Muponyeshe wagonjwa, mufufue wafu, mutakase wenye ukoma, mufukuze pepo. Mulipokea bure, mutoe bure vilevile.


Yoane akawajibu: “Hakuna mutu anayeweza kuwa na kitu isipokuwa amekipewa na Mungu.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Wala wasikuwe na urizi kati ya wandugu zao; Yawe ndiye urizi wao kama vile alivyoahidi.


Hakuna mutu anayejipatia heshima hii ya kuwa Kuhani Mukubwa yeye mwenyewe. Lakini anapaswa kuitwa na Mungu, kama vile Haruni alivyoitwa.


Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Musitawale kwa kinguvu kundi lile lililowekwa chini ya uangalizi wenu, lakini mukuwe mifano kwao.


Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ