Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.
Wao watafanya kazi utakazowapa na kutimiza mapaswa yao juu ya hema. Lakini hawana ruhusa ya kugusa vyombo vya hema, wala kukaribia mazabahu, kusudi wasikufe, nawe vilevile usikufe.
Kutoka katika lile fungu la jamii nzima, utwae mumoja kati ya kila makumi tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo na mbuzi. Hivyo utawapa Walawi ambao wanashugulika na kazi katika hema la Yawe.
Lakini, anaweza kuwasaidia Walawi wenzake wanapotumika katika hema, lakini haruhusiwi kufanya kazi yoyote peke yake. Ndivyo utakavyowapangia Walawi kazi.
Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.